KURAAN 2:125.
Na kumbukeni tulipo ifanya ile ALKAABA iwe pahala pa kukusanyikia watu na pahala pa amani. Na alipo kuwa akisimama Ibrahim"MAKAAMU IBARAHIIMU" pafanyeni pawe pa kusalia. Na tuliagana na Ibrahim na Ismail: Itakaseni Nyumba yangu kwa ajili ya wanao izunguka kwa kut'ufu na wanao jitenga huko kwa ibada, na wanao inama na kusujudu.


KURAAN 2:126.
Na alipo sema Ibrahim: Ee Mola wangui! Ufanye huu uwe mji wa amani, na uwaruzuku watu wake matunda, wale wanao muamini ALLAH na Siku ya Mwisho. Akasema: Na mwenye kukufuru pia nitamstarehesha kidogo, kisha nitamsukumiza kwenye adhabu ya Moto, napo ni pahala pabaya mno pa kurejea


KURAAN 2:127.

Na kumbukeni Ibrahim na Ismail walipo inyanyua misingi ya ALKAABA wakaomba: Ewe Mola wetu! Tutakabalie! Hakika Wewe ndiye Msikizi Mjuzi.


KURAAN 2:128.
Ewe Mola wetu! Tujaalie tuwe ni wenye kusilimu kwako, na pia miongoni mwa vizazi vyetu wawe umma ulio silimu kwako. Na utuonyeshe njia za ibada yetu na utusamehe. Bila shaka Wewe ndiye Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.


KURAAN 2:129.
Ewe Mola wetu! Waletee Mtume anaye tokana na wao, awasomee Aya zako, na awafundishe Kitabu na hikima na awatakase. Hakika Wewe ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hikima.

Views: 1336

Kurasa: Islam, Mawaidha, Quraan

Andika Salamu

Lazima uwe mwanachama wa Zanzibarwebsite ili uweze kuweka ujumbe!

Join Zanzibarwebsite

Maoni ya NASSER on August 24, 2009 at 7:47am
Tunamuomba ALLAH Mafanikio Tuwe Uma Mmoja Katika Ridha Yake ALLAH Aamin
Maoni ya IL-YA on April 1, 2009 at 1:18am
HII AYA YA MWISHO INASEMA KAJA (S.A.W) KUTUFUNDISHA KITABU NA HEKIMA,NA WATU WANAOTUFUNDISHA KITABU NA HEKIMA WALIOFUNDISHWA NA MTUME (S.A.W) WAKANYESHWA ELIMU IKAJICHANGANYA NA DAMU YAO,NI AHLUL BAYT WAKE (A.S),HIVYO LAZIMA TUREJEE KWAO ILI TUWEZE KUIPATA ELIMU BORA NA MAFUNDISHO BORA,KWANI WAO WAO NDIO WANAOIJUA QUR'AN NA NDIO WALIOJAZWA HEKIMA NA MTUME (S.A.W) WATU AMBAO QUR;AN IMETEREMSHWA KATIKA NYUMBA YAO.WAO NDIO WALE WALIOKUWA NA ELIMU YA KITABU,(KAFAA BILLAH SHAHIIDA,BAYNIY WA BAINAKUM ,WAMAN INDAHU ILMUL KITAABU),

WAMAN INDAHUU ILMUL KITAAB,YAANI IMAM ALI (A.S) NDIYE ALIYEKUWA NA ILMUL KITAAB,KAMA UNABISHA REJEA TAFSIRI YA AYA HII KISHA TWAMBIE MTUME (S.A.W) ILIPOSHUKA ALISEMA NI NANI ALIYEKUSUDIWA KUWA NDIYE ALIYEKUWA NA ILMUL KITAAB????????SI ABUBAKAR KUWA MAKINI WALA UMAR WALA UTHUMAN,USIJE NA MAAJABU,UTACHEKWA!!


THE SO CALLED ..IL-YA..


TH SO CALLED ..IL-YA..

© 2012   Created by zanzibarwebsite.com.

Lebo  |  Report an Issue  |  Terms of Service