NAPENDA PASI KIFANI BUSHAKO NIMASHAKANI
NAPENDA KIFUANI NATEREMKIA MAPAJANI
NAPENDA MI PUNGUANI CHA MSINGI NAUMIYAA
NAPENDA UMBO LAKE NYWELE ZAKE KADHALIKA
NAPENDA SAUTI YAKE RANGI YAKE KUCHANGANYIKA
NAPENDA HARUFU YAKE MANUKATO YAKE YANIWEWEZEKA
NAPENDA AKICHEKA NINAPO MFURAHISHA
NAPENDA AKIPEPESUKA HADI NGUVU ZINAMUISHA
NAPENDA AKIWEWESEKA ELIMU NIKIMFUNDISHA
NAPENDA NAPATA WAZIMU NASEMA KWA UFASAHA
NAPENDA NAHISI KUZIMU NA WALA SIFANYI MZAHA
NAPENDA MUSINILAUMU NAUGULIA MAJERAHA
NAPENDA SISHAURIKI NA WALA SITAJUTA
NAPENDA HADI CHUKI KWA KILA ANAYEMUITA
NAPENDA KIHAFUBEKI ANIPITAE NAMVUTA
NAPENDA NA SITAKI WOTE WANAONIBEZA
NAPENDA WAKIHAMAKI VIGAE WAWEZA MEZA
NAPENDA WAKINISHTAKI KUNIFUNGA MUNAWEZA
NAPENDA KIARABU KISWAHILI NISHAPITA
NAPENDA MUHIBU NA CHAKULA NISHAPIKA
NAPENDA SINA AIBU BUSHAKO NIMESIKIKA.
Kurasa:
Penda wangu upendavyo Jua kuna mwisho wake
Vizuri uvionavyo Mpambaji Mola wake
Leo tamu kesho ovyo Huyo huyo utamke
UPO
Weka akili timamu Kelele zisijezuke
Ujue na kufahamu Kwa hayo na uridhike
Wengi wamejihujumu Subiri watu wacheke
UPO !
Bushako umahashumu Nadhari bora uweke
Tafakari Muadhamu Usiyarushe mateke
Kwaheri pendo lidumu Tulia usisumbue
Ya KUONANA !
Huyo Babengwa Akupendae !!! hahahaa....
Permalink Imejibiwa na Swaleh Suheil Abeid on February 9, 2012 at 10:32am Mahaba huwa adhimu, mno yakikulekeya
Tena yanakuwa tamu, nyonda zikiendeleya
Mara yanakuwa sumu, siku yakikuzingiya
Tafakari muadhamu!
Nakuonavyo wasota, katwani humakiniki
Wastahabu kutota, maneno huambiziki
Mahaba yaliyoota, ni shida hayakungoki
Nakuombea salama!
Mahaba hukuliwaza, kwa furaha ukawanda
Mwisho yajakutukiza, mwili wako ukakonda
Bushako nakueleza, usidhihaki na nyonda!
Nakunasihi Bushako!
Mahaba yana dharubu, Bushako uniamini
Yana mengi masaibu, si leo toka zamani
Kwa pendo lilokuswibu, naomba uwe makini
Kwa heri ya kuonana!
Nduguyo: Swaleh Suheil Abeid (Sauti Ya Haki)
Permalink Imejibiwa na bushako on February 11, 2012 at 9:25am swalehe na babengwa , nyote nawasikiliza
bushako hajawa bingwa, nasoma sitawabeza
nyumba ikawa kungwa, mukachoka kunisemeza
iki taka kula chungwa , uchachu utaumeza
bushako msema kweli , kusini na kaskazi
jambo kwake halifeliii, ugumu wa kiangazi
kwa penzi amekubali, hata kuwa mpagazi
kulikwepa ni muhali, nabembeleza mapenzi
Permalink Imejibiwa na Swaleh Suheil Abeid on February 11, 2012 at 12:03pm Sio kua ni sharuti, kukupa njema kauli
Kwa pendo lilozatiti, zakukumba idhilali
Bora mche Jabaruti, upate sitiri hali
Rakataini uswali!
Hebu mwepuke bilisi, pendo liwe la halali
Jiandalie harusi, suna ya wetu Rasuli
Heri uowe upesi, ukondoke mushikili
Nakuombea sahali !
Bushako sinilaumu, kukupa wangu ukweli
Ndoa kwako ni muhimu, takubariki Jalali
Ingawa mi si imamu, nakuombea sahali
Kaowe binti halali!
Nduguyo: Swaleh Suheil Abeid 'Sauri Ya Haki"
© 2012 Created by zanzibarwebsite.com.