naanza kwa bashasha, maneno yangu kutoka
nimeijaza bahashaaa, pomoni hadi kufika
dhamira yangu tamasha, mchumba kwenda mposa.
mahari nimeshaweka , hilo kwangu halina shaka
begi nimeshaliwekaa, nyumba rangi nishapakaa
mke jamani namtakaa, kiudhati hasa natamkaa
natafuta mshenga akifika, ruhusa kwao naitafuta.
mshengaaa ukifika , ujumbe wangu fikishaa
mwera njia ya chwaka, nyumbani kwa baba aisha
siku saa dakika ikifikaa, muda mzuri baada ya isha
usijivishe makabokaa, mshenga nanakufundishaa.
mahari kidogo upatane, dunia imeharibikaa
isifikie hata laki nanee, tuwasiliane kukuharibika
mtoto mwari siye mjane, hakuvimba kama pakaa
wanasema namba nane, mshenga usijebabaishwa.
mshenga ukienda lazimisha, ifanyike akdi haraka
watu wote nitahamasishaaa, inshallah kharusi itafika
jimai bushako nitakamilishaa, hehehe nitazaa kama paka
mshenga tena nakuharakisha, wengine waweza nipita.
ni bushako, bushakire, bushakirina,
Kurasa:
© 2012 Created by zanzibarwebsite.com.