MAKOMBO !!

Kila alae makombo   Hujiona kafaidi

Wewe ulie mrembo   Hili usilikaidi

Walionasa urimbo     Wanalijua zaidi

HUJIONA KAFAIDI  KILA ALAE MAKOMBO

Tembea ufike ng'ambo   Tena uweke juhudi

Useme chako kimombo   Sudi umwite Juedi

Kujitanda kwa mapambo Makombo uyafaidi

KILA ALAE MAKOMBO  HUJIONA KAFAIDI

Yana nini majigambo     Asazae kafaidi

Huna lako tena jambo   Wa awali kakuzidi

Nimeyafumbua mambo   Wazi iwe makusudi

HUJIONA KAFAIDI  KILA ALAE MAKOMBO

Kata mti iwe fimbo             Tengeneza mjeledi

Yake thamani makombo       Chake cha shibe uledi

Nahodha kwakwe ni chombo Makombo kuwa baidi

KILA ALAE MAKOMBO  HUJIONA KAFAIDI

Hitimisho langu jambo       Na ukome ufisadi

Mambo yaendao kombo     Yameingia kuadi

Leo nishaimba wimbo        Kiitikio menadi

HUJIONA KAFAIDI  KILA ALAE MAKOMBO

Views: 148

Jibu Hii

Majibu ya Mjadala huu

hehe, hehe, hehe, hehe.     haha , haha, haha, haha. 

ni na cheka kwa dhihaka.     babengwa   limekufika.

wewe panya mimi  paka.     moyo wako umevurugika.

ongoza njia uking'aka.          makombo wenzio twayataka.






nakuhisi   una   jambo.       ila kulisema hutaki.

kuyaponda   makombo .     hakuna ila umehamaki.

wapi yako majingambo.    mtoto ninaye kiembe samaki.

siyajali yako mafumbo.     nitakualika siku yakula keki.







makombo huwa makombo.    ikiyashiba na vinywaji.

lakini hili la mwanakombo.     umelikosa kwa ujuajii.

ulijifanya wewe  ni mbogo.     kutembezwa kwa vibajaji.

umekuja na wako ungooo.      utawezaje kuyaweka maji ?







kwangu wala si makombo.     walitambuwa kwa hakika.

naijiiibu  yako  hii  tungo.        waweza uka  kasirikaaa.

huyu binti ana maungoo.        umehumiwa bila shakaa.

bushako ala hana maringo.     babengwa utaishia kubweka.





bushako bushakirina... 

mmh!

mla hasa mla leo, mla jana kala nini,

fakhariye simulio, yungali njaa tumboni,

mla na maendeleo,leo ana kitu gani,

kala nini mla jana,

                mla hasa mla leo!

haja mkidhi sihaba,hatokoti maungoni,

mla leo akashiba, fakhariye shukurani,

wajana wake msiba, hana leo mkononi,

kala nini mla jana,

                 mla hasa mla leo!

huyajutiya makombo, kayasaza kulikoni,

aloyapiga kikumbo,kwa isirafu mezani,

leo bakuli na chombo, atafuta muhisani,

kala nini mla jana,

                mla hasa mla leo!

anatetema baridi, joto halipo mwilini,

anatamani yarudi, makombo kwenye sahani,

kama jana kafaidi, leo karaha, huzuni,

Kala nini mla jana,

                 mla hasa mla leo!

nakaditama Dikupa, tano siyo khamsini,

ila si vyema kutupa, ingali ina thamani,

japo kipande mfupa, kina mchuzi jikoni,

kala nini mla jana,

                 mla hasa mla leo!

Dikupa Dikupatile dikilema (cheko lenye afya)

Wacheka nini mchekwa , Bushako umepagawa

Babegwa alokwitika . hakuna wa kukutuwa

nyamaza sije tapika,  Makombo yakakuuwa




Babegwa hasara yako, thamani umejitoa

unachekwa na wenzako, makombo ulovamia

chagua chaguo lako, umeondoka na chua



Babegwa utabakia,  kuchekwa na kuzomewa

Kipitacho kurukia,    Mwisho watakuondowa

Bushako achekelea, yupo kwake amepowa

 

Babegwa hutahayari?  huna lako lilikuwa

Wanifanya nighairi, kuandika yangu nia

kanuni huzikariri, Makombo wayavamia


A'malik

Shirika la kiswahili Halina zake inadi

Shida ikikukabili    Kwao kicheko huzidi

Hukupetea kabali  Fedhuli hutaradadi

POLE KWAO HAWAJALI

 

Kama hili hukubali     Tizama hao wawili

Fadhila hata kwa hali Waniwekea kufuli

Nani ataekubali         Shirika la kiswahili ?

KWAO POTELEA MBALI..

 

Makombo ukiwa huli  Hilo lina afadhali

Nimekoma ufedhuli    Nyie msioniojali

Zipunguzeni shughuli Wa moja havai mbili

CHEI CHEI YENU !!

Wakiambiwa ukweli, hujifanya kuhamaki

Wasingizia kiswahili, Batili iwe ya haki

tulia nikupe ukweli, sipate taabu na dhiki.





Hasira mwisho hasara, Faraha mwanzo hilaki

Usijitie papara, Mkali huambiliki

Uamuzi wa hasira, Wewe mtu si samaki.





Kwangu mimi ni furaha,   Mkizi ukihamaki

Huona nyota ya jaha,  Navua bila mikiki

Wacha nile zangu raha, Nimeekewa na keki.








Bebegwaa ......Punguza Jazba    hahahahahaha

Kipi kingekupotea           Pole kumpa mfiwa

Nini ungekikosea             Mja nikafarijiwa

Ndo kwanza wakichochoa Kidonda kinachopowa ?

POLE !!

Ungeliitwa fisadi       Kelele unaonewa

Au wafanya kusudi    Nipate kulaumiwa

Hamaki na ukaidi       Kipi utachochaguwa

POLE !!

Haluwa haina makombo jamani

Yategemea kayaacha nani, halua iliyo makombo ya mlevi au mtoto - mmh! hayaliki huwa uchafu spider !!hahahaah

RSS

© 2012   Created by zanzibarwebsite.com.

Lebo  |  Report an Issue  |  Terms of Service