januwari 12 juwa kuchomoza zanzibar huru sasa jina tanzania . kweli ?

kweli wazanzibari wako huru ?

Views: 37

Jibu Hii

Majibu ya Mjadala huu

UHURU WABENDERA lakini tangu mwaka 1964 hakuna bendera mpaka mwaka 1995 nabendera yetu ina masharti hairuhusiwi kupepea nje ya zanzibar .kwaupande wa zanzibar bendera inaitwa KIKOI .tunaumia na kusononeka maungoni wetu kuwa bendera yetu imefungwa jela visiwani
swali langu kwanini wanzanzibar wabaguzi
JAMANI INAKUWAJE WANZANZIARI WANACHUKUA WABARA KWA NINI


jaa alisema:
swali langu kwanini wanzanzibar wabaguzi
kwa sababu wana ugabachori flani, na magabachori wote wabaguzi.

jaa alisema:
swali langu kwanini wanzanzibar wabaguzi
Wa Zanzibar Si Wabaguzi Ndugu Yangu wazanzibar ni wakarimu sana.
Lakini hii leo maji yamezidi unga ndoo maana huruma imekimbia ubaya umetawala, kwa sababu hapa tulipo leo tumefikishwa. Kumbuka nyuma tulipotoka huruma ya wazanzibar kwa ndugu zao wabara lakini leo wanavyowatesa. Ukitaka usitake wazanzibar ndoo walo wastaarabisha wabara na mpaka leo tunaendelea kuwastaarabisha hatuchoki sisi. Rudi nyuma kwenye historia utauona mchango wazanzibar kwa wabara iweje leo utuone wabaguzi? Leo hapa tulipofikia tumefikishana sote kama wabaguzi ni sote. Maana udugu gani huu mwenzio anajanga si lakutarajia ( Tatizo la Umeme Zanzibar) unashindwa kumpa msaada huu kama si ubaguzi ni nini ? Hivi majuzi tuu siku ya alhamisi iliyopita katika Bunge la Tanzania Waziri mkuu Mizengo Pinda alijibu maswali katika mtindo wa papo kwa papo akatupiwa suali la umeme zanzibar aliulizwa: Serikali yake ya Muungano imetoa msaada gani kutatua tatizo la umeme zanzibar ? alichojibu ndoo kwanza anafikiria kukutana na wizara ya fedha aone ataisaidia vipi zanzibar! Tatizo liko miezi miwili nyuma yeye ndoo kwanza anafikiria! huu ni ubaguzi na kejeli juu anayoifanya kiongozi wa ngazi za juu katika nchi. Hata katika Sakata la ukozi wa MV Fatihi pia tuliona kejeli siku tatu baada ya tukio ndio ikaja Meli ya Ndovu kuja kusaidia jitihada za uokozi! Jeee Mmesahau nyie tulivyokupeni waokozi kuja kuokoa katika tukio la MV Bukoba? Nani Mbaguzi wa Mwenziwe ?
Mmetusomesha sasa tushaelimika tuwacheni tutumie elimu yetu. Alaa kumbe mkuki kwa zanzibar mtamu kwa Tanganyika mchungu?

jaa alisema:
swali langu kwanini wanzanzibar wabaguzi
Zanzibar Haiko Huru
Zanzibar imetawaliwa na wakoloni weusi kutoka Tanganyika.
kumbukumbu ya wazanzibary kwa wale walio jitolea kufanya maafa yasio sahaulika daima

HII NI SIKU YA HUZUNI

Na V sign ilitumika kuwalazimisha waliofungwa kwenye Magereza wakati wa Mapinduzi.

 Nyerere na Muengereza aliwapiga picha na kusambaza ulimwenguni kote kama dalili ya kuwa Mapinduzi yamefanywa na wananchi wote wa Zanzibar.

Unajuwa wakati wa Mapinduzi Waislamu( si kusudii kama walikuwa Waarabu peke yao ndio waliowekwa vizuizini bali ni waislamu )hapakuwa na Mkristo hata mmoja ndani ya Magereza wakati wa Mapinduzi.
Walikuwa wakilazimishwa kounyesha Sign ya V na kuambiwa lazima wacheke halafu hupigwa picha na kusmbazwa Ulimwenguni ili Waengereza waonyeshe kama kwamba wanachi wamefurahikia Mapinduzi ya kumpindua sultan.
Na unajuwa kama wakikataa kuonyesha Sign ya V walikuwa wakifanywaje?

Walikuwa wakipewa adhabu na kuuliwa na wengi wao masikini walikubali ili wasalimishe roho zao. na walokataa walikuwa wakipigwa risasi au kutiwa vitanzi.  Inshallah atawaingiza Peponi kwani walikufa Mashahidi.

Napenda na mimi nitoe mchango wangu.

 

Sura ya Mapinduzi ya Zanzibar ina mtizamo wa nje na ndani.

Ki nje ni kuhalalishwa umuhimu wa tokeo kuwa kweli wazanzibari walichokoa na kutawaliwa na hatua ya mapinduzi yao kumng'oa utawala wa kisultani na kutandika taifa huru lenye mamlaka ya kujiendeshea nchi yao bila ya amri kutoka nje ya utawala huo.Mapinduzi haya ,yalisomeshwa katika skuli ili watoto waelewe hivyo na kutukuza siku hiyo kuwa ni siku ya Ukombozi wa visiwa vyetu chini ya Chama Afro Shirazi Party.

Ki ndani ,wazanzibari wenyewe ndio waliopinduliwa kwani tayari ,Zanzibar ilikuwa taifa huru - kupitia uchaguzi wa kuwa serikali ya mseto- 9desimba 1963.Kilichozuka ni kuangushwa kwa taifa hilo.Ndio Mastermind akiwa ni Muingereza.Ajabu yake hakutimia hata mwaka 26 Aprili 1964, kuzaliwa Muungano na kuwa nchi - Tanzania.Na ndio kabali ya Zanzibar kuanzia muungano wa nchi mpaka kufikia ni sehemu tu ya Tanzania.

 

Kama faida ipo hapo na kama hasara iko hapo.

 

Machache ,yangu ni hayo.

Ahsante Babengwa huo ndio ukweli, Ilikuwa ni Mastermind ya pekee ya kuiondosha zanzibar katika hadhi ya dunia.

Muengereza aliiuwa zanzibar kidogo kidogo na hatimae kuimaliza.

suali ni hili jee zanzibar itarejea na kujiamulia wenyewe?

Mwenyeezi Mungu ndie Mjuzi wa kweli.

wazanzibary au watanzania ndio wanaosherehekeya kwa siku yao ?

RSS

© 2012   Created by zanzibarwebsite.com.

Lebo  |  Report an Issue  |  Terms of Service