washauri nauliza , akili yanizunguka
usewaza nimeuliza, jawabu sijalipata
nimepita pia bakiza, pamoja na bakita
cheupe cheusi kwanza,bushako vinanitanza.
viwili nimefishika , mikononi ninavyo
kuna watu wavitaka, kwenda navyo bagamoyo
njia panda nimefika, nauuumiza wangu moyo
nambieni kwa hakika, ninavyo shaurimoyoo.
cheusi chanipendeza, na cheupe kadhalika
kuviacha sitaweza , maini yanikatika
napigwa kama pweza, kijasho kinanitoka
mwenzenu nikwenye kizaa, mwanga wenu wahitajika.
bushako bushakirina
Kurasa:
© 2012 Created by zanzibarwebsite.com.